![]() |
| Malala akihutubia |
MALALA YOUSAFZAI ambaye
alipigwa risasi kwenye kichwa na wanamgambo wa Taliban nchini Pakistan miaka
miwii iliopita anazuru mji mkuu wa Abuja nchini Nigeria ili kuendeleza kampeni
yake ya elimu bora miongoni mwa wasichana na wanawake.
Aliwasili mjini humo
akisheherekea mwaka wa 17 wa kuzaliwa kwake miezi mitatu baada ya zaidi ya
wasichana 200 wa Nigeria kutekwa nyara na kundi la Boko Haram.
Katika taarifa yake, amesema kuwa ziara yake
nchini humo ni kuwaenzi wasichana hao ambao walijitolea kupata elimu.Malala alipigwa risasi kwa kuwa alikuwa anaongoza kampeni ya wasichana kupata elimu nchini Pakistan na baada ya kupona kwake nchini Uingereza aliapa kuendelea kampeni hiyo.
Ni nusu ya wasichana waliokuwa kati ya umri wa miaka sita na kumi na moja ambao huenda shule nchini Nigeria,licha ya kutajwa kama uchumi mkubwa barani Afrika.

No comments:
Post a Comment