WANANCHI wa kata ya mabura wilayani Kilosa Mkoani
Morogoro wameamua kutengeneza Barabara zinazozunguka kata hiyo ili kukabiliana
na changamoto ya usafiri inayowakabili
.
Akizungumza na Mbiu ya Maendeleo
mapema leo Diwani wa kata ya Mabura Meshack Chalo amesema kuwa wananchi
wameamua kuchonga barabara hizo kwa kutumia majembe na mapanga kutokana
na adha ya usafiri wanayopata.
Chalo amesema kuwa wananchi
wamejitolea kuchonga zaidi ya Kilometa 17 za barabara ya kutoka kijiji cha
mabura kwenda mbili yenye urefu wa kilometa 5, mbili – kagera kilometa 4,
Mtumbatu hadi mbili kilometa tano na mbili – mavungani kilometa tatu na
kuongeza kusema kuwa kwa mara ya mwisho barabara hizo Kuchongwa ni mwaka 1974.
Amesema kutokana na Ubovu wa
barabara hizo kumepelekea wananchi kushindwa kusafirisha mazao yao kwenda
kwenye masoko hali inayosababisha kushuka kwa uchumi wa kijiji na
maendeleo kurudi nyuma.
Aidha Chalo ameleza kuwa kutokana na
jitihada zinazofanywa na wananchi wa kijiji hicho mpaka ifikapo mwishoni
mwa mwezi wa saba atahakikisha barabara hizo zinapitika na kwmba anaiomba
serikali iwaunge mkono kwa kuchangia ukarabati wa barabara hizo kwani wananchi
hao wana haki ya kupata hitaji msaada kutoka serikalini kwkuwa walipakodi wa nchi
hii.
No comments:
Post a Comment