Monday, June 2, 2014

WIZARA ya maji yatakiwa kuhakikisha kuwa miradi ya maji inakamilika ili kuondoa adha kwa wananchi


SERIKALI  ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kupitia wizara ya Maji imetakiwa kuhakikisha miradi ya maji inakamilkika kwani maeneo mengi nchini hayana huduma ya maji.

Wito huo umetolewa na wabunge mapema leo Bungeni mjini Dodoma wakati wa kujadili bajeti ya wizara ya maji kwa kuitaka wizara hiyo, kukamilisha miradi ya maji kwernye maeneo mbalimbali hapa nchini.


Mbali na hayo Wabunge wameitaka wizara ya maji kuanzisha mfuko wa maji ili uweze kupunguza urasimu katika utekelezaji  wa miradi mbalimbali ya maji  kama ilivyo mifuko ya barabara na umeme.

Mipango ya serikali ni kuwa ifikapo mwaka 2015 aasilimia 95 ya watu wa vijijini wawe wamepata maji safi na salama hali inayokwenda kinyume na mikakati na malengo hayo kwani mpaka sasa ni asilimia 65 tu ndio wanapata maji safi na salama

No comments:

Post a Comment