Sunday, June 1, 2014

WANANCHI wilayani Kilosa watakiwa kutoa taarifa kwa mganga mkuu pindi kukitokea lugha chafu toka kwa wahudumu wa afya



KAIMU  mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Kilosa,mkoani Morogoro Dokta CHIWEKA  ametoa wito kwa wananchi wakiwemo wazee kutoa taarifa ofisini kwake endapo watatolewa lugha chafu hospitalini mara wanapokwenda kupata huduma ya matibabu.

Dokta  Chiweka ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akizungumza na baraza  la wazee la mjini Kilosa kufuatia malalamiko yaliyotolewa  na wazee hao kuwa watumishi wa idara ya afya huwanyanyasa pindi  wafikapo hospitalini  kupata matibabu.

Akijibu mnalalamiko hayo,Dokta Chiweka  amesema ameyapokea kwani alikuwa hafahamu kama watumishi wa idara ya afya wanatabia ya kutoa lugha chafu kwa wagonjwa hospitalini hapo hivyo amewataka kutoa taarifa ofisini kwa mganga mkuu ili wahusika wachukuliwe hatua .

Kumekuwepo na malalamiko kuwa baadhi ya watumishi wa ihospitali ya wilaya ya kilosa wanatabia ya kuwatolea lugha chafu wagonjwa wanapokwenda kupata matibabu.










No comments:

Post a Comment