Sunday, June 1, 2014

WAKULIMA wilyani Kongwa waipongeza idara ya kilimo



MAAFISA ugani wa kilimo katika wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, wamepongezwa kwa kutoa elimu na kuwahimiza wakulima katika vijiji mbalimbali vilivyopo wilayani humo kulima mazao yanayostahimili  ukame ilii kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.


Wakiongea na mbiu ya maendeleo hapo jana wakulima wa vijiji vya Ngambi , wameeleza kuwa katika msimu wa kilimo kwa mwaka huu wana uhakika kupata  mtama mazao mengi yamatama kutokana na kusikiliza utaalamu toka kwa maafisa kilimo wa kata na wilaya.

Wamesema , endapo hali ya ushirikiano kati ya wataalamu wa kilimo na wakulima utaongezeka utasaidia kupunguza tatizo la uhaba wa chakula unaoikumba vijiji vingi wilayani humo  mara kwa mara kutokana na wakulima wengi kutozingatia kanuni za kilimo  boracpamoja na baadhi ya wataalamu kushinda ofisini na kutowatembelea wakulima kwaajili ya ushauri bora.

No comments:

Post a Comment