Monday, June 2, 2014

KAMANDA wa polisi mkoani Morogoro apokewa kwa mabango na watoto wanaoishi katika mazingira magumu



KAMANDA wa polisi Mkoani Morogoro juzi katika maadhimisho ya siku ya mtoto alipokelewa na watoto wanaoishi katika mazingira magumu Manispaa ya Morogoro kwa mabango yenye ujumbe mbalilmbali ukiwemo unaomtaka kuweka kitengo maalumu cha watoto katika taasisi yake.
 
Ujumbe huo uliomshawishi mwakilishi wa kamanda huyo Clemence Matata kutoka dawati la kupinga unyanyasaji wa kijinsia na ukatili kwa watoto ulikwenda sambamba na laana dhidi ya vitendo vibaya wanavyotendewa kila kukicha huku kukiwa hakuna hatuia zinazochukuliwa dhiidi ya wahalifu.

"watoto tunauwawa,tumekuwa chambo kukidhi haja za kimwili kwa watu wazima wakiwemo ndugu zetu,ushirikina na yote haya yanafanyika kuwa hatuna wa kututetea kwakua serikali haitujali...tunaomba serikali itutengenezee mazingira bora ya usalama na hadhi zetu"alisema Veronica Omari.

Akijibu baadhi ya madai hayo kwa niaba ya Kamanda,Matata alisema jeshi la polisi limekuwa mstari wa mbele kupambana na unyanya saji huo kwa watoto na jinsia laikini limekuwa likikabiliwa na changamoto ya kukosa ushirikiano kwa jamii.








No comments:

Post a Comment