Monday, June 2, 2014

SERIKALI wilayani Rombo yaunda kikosi kazi maalum cha kukabiliana na wazazi wa watoto ambao hawajaripoti shule


SERIKALI  wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro imeunda kikosi kazi maalum cha kukabiliana na wazazi ambao watoto wao hawajaripoti shuleni kuanza kidato cha kwanza mpaka sasa licha ya kwamba wamechaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari, zoezi ambalo limeelezwa kuanza kuleta mafanikio makubwa.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo mkuu wa wilaya ya Rombo Elinasi Palanjo amesema maamuzi ya kuanzishwa kwa kikosi hicho yametokana na kuwepo kwa  idadi kubwa ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na sekondari  kidato cha kwanza, kushindwa kuripoti katika shule walizopangiwa.

Bw Palanjo amesema ,baada ya kufuatilia waliweza kugundua kuwa, jumla ya watoto  3411 ndiyo walioripoti kati 4332, waliochaguliwa kujiunga na sekondari kidato cha kwanza,huku watoto 732 hawakujulikana walipo hali iliyoilazimu serikali wilayani huo kuanza zoezi la kuwasaka watoto hao.

Nae Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Rombo Bw Judathadeus Mboya, amesema baada ya serikali kuona kuwa mahakama imeshindwa kuwatia hatiani wazazi hao  ,halmashauri imetunga sheria kwa kutumia kifungu kidogo cha kumlinda mtoto ambapo baada ya kutunga sheria hiyo, jumla ya wazazi 38 wamefikishwa katika mahakama za mwanzo zilizoko katika tarafa hiyo.

Wazazi waliokamatwa kwa kushindwa kuwalipia watoto wao ada ya kidato cha kwanza, wamefikishwa katika mahakama za mwanzo zilizoko katika tarafa hiyo na kuswekwa rumande kwa muda wa wikimbili kila mmoja    





No comments:

Post a Comment