HALMASHAURI nchini zimetakiwa kuendelea kutenga
asilimia kumi ya mapato ya ndani kwa ajili ya kuchangia mfuko wa
Maendeleo ya
wanawake ili kuwawezesha wanawake wengi zaidi kupata mikopo yenye
masharti nafuu kupitia mifuko hiyo ikiwemo vikundi vya vijana
Agizo hilo limetolewa jana na Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi na
Mjumbe wa Kamati kuu ya CCM Taifa,bwana Abdalalla Bulembo katika vikao
vya Halmashauri kuu ya CCM wilaya za Kilwa,Liwale,Nachingwea na Ruangwa katika
ziara yake inayoendelea mkoani Lindi.
Bwana Bulembo amebainisha kuwa maendeleo katika nchi na jamii yoyote yanaanza
na wanawake na kwamba mwanamke akiwezeshwa na kuonyeshwa fursa za kujikomboa
kiuchumi anaweza kuleta mabadiliko makubwa katika familia na jamii nzima, hivyo
ni wajibu wa halmashauri kuwawezesha wanawake kiuchumi ili kutekeleza
sheria ikiwemo utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Katika ziara hiyo ya kukagua utekelezaji wa ilani unaofanywa katika mkoa
huo pia amekagua miradi mbalimbali ya Jumuiya ya wazazi na Vikundi
vya Vijana na Jumla ya wanachama 1200 walijiunga na CCM ikiwemo
wengine toka vyama vya upinzani
No comments:
Post a Comment