WACHOMA mkaa kutoka Tarafa ya Ulaya ,wilaya ya Kilosa,
mkoani Morogoro wameiomba serikali kuruhusu vibali vya kusafirisha mkaa
vitolewe katika ngazi ya vijiji ili kuweza kuwaongezea kipato ambacho
kitawasaidia kukuza uchumi wa wananchi, kijiji na Taifa kwa ujumla.
Wakiongea
na mbiu ya maendeleo wachoma mkaa hao na viongozi wa vijiji na wachoma mkaa hao na viongozi wa vijiji
wamesema kuwa hivi sasa kibali cha
kuchoma mkaa hutolewa wilayani kwenye ofisi za maliasili
pekee kitu ambacho kinawapa ugumu kupata kutokana na gharama za usafiri
kwenda wilaya na umbali uliopo hivyo hivyo kutumia gharama kubwa kukipata
na kusababisha kuuza kwa bei hasara.
Mmoja
wa wachoma mkaa Stella Makubi mkazi wa kijiji cha Msimba kata ya Mikumi ,
amesema wamepata mafunzo kutoka TFCG na Mjumita ya uchomaji mkaa na sasa
wanazalisha mkaa mwingi lakini wanashindwa kuuza kwa bei nzuri kutokana na
utaratibu wa utolewaji wa vibali vya kusafirishia kutolewa wilayani hali
inayosababisha usumbufu mkubwa kukipata hivyo wanaiomba serikali kuweka
utaratibu wa vibali hivyo kutolewa kwenye ngazi za vijiji.
Akizungumza
na waandishi wa habari Mwenyekiti wa kijiji cha Ulaya Mbuyuni Hamisi Rashidi
Mjomba ameyapongeza Mashirika ya TFCG na Mjumita kwa kushirikiana na serikali
kuona umuhimu wa kurudisha umiliki wa misitu kwa wananchi na ameomba serikali
kuruhusu vibali vya kusafirishia mkaa vitolewe kwenye vijiji.
No comments:
Post a Comment