SERIKALI imesema itawachukulia hatua viongozi wa vijiji na kata
wanaokaidi kusoma mapato na matumizi ya michango ya miradi mbalimbali ya
maendeleo inayochangwa na wananchi katika ngazi ya kijiji.
Hayo
yameelezwa mwishoni mwa na Naibu Waziri
wa Tawala za mikoa na serikali za mitaa(TAMISEMI ) Agrey Mwanri wakati akijibu
swali la nyongeza la mbunge wa viti maalumu Kristowaja Mtinda wa chama cha
CHADEMA aliyetaka kujua hatua zitakazo chukuliwa kwa watumishi hao
wanaosababisha wananchi kuacha michango kwa kukosa taarifa.
Mwanri
amesema michango katika vijiji na halmashauri inafanyika kwa kibali cha
serikali kinachopatikana kwa mkuu wa Wilaya na kwa mujibu wa sheria ni lazima
mapato na matumizi yatolewe kwa wananchi kwa kubandikwa ubaoni.
Katika
swali la msingi la mbunge wa Tandahimba , Juma Njwayo wa chama cha mapinduzi
alitaka kujua serikali ina mpango gani wa kusaidia halmashauri ya Tandahimba
ili kituo cha afya walichojenga kiweze kutoaa huduma bora kwa wananchi.
Amesema
Zahanati hiyo ina watumishi watatu , muuguzi mmoja na wahudumu wa afya
wawili, nyumba moja ya mganga na jengo moja la matibabu ya wagonjwa wan
je (OPD) ambalo linaendelea kujengwa na limefikia asilimia 85 ya utekelezaji na
kusema kuwa katika bajeti ya mwaka 2014/2015 serikali imetenga kiasi cha
shilingi milioni 53.6 kwa ajili ya awamu ya pili ya ujenzi wa wodi hiyo.
No comments:
Post a Comment