Thursday, August 7, 2014

MAONESHO ya nanenane iwe chachu yakutekeleza mipango mkamambe ya kilimo


Mtaaalamu wa kilimo akitoa maelezo viwanja vya nanenane  Morogoro

MAONESHO ya wakulima yanayofanyika kila mwaka ifikapo tarehe 8, mwezi wa nane iwe chachu ya kutekeleza mipango kamambe ya limo hasa ule ulioasisiwa na Rais  Jakaya Kikwete mkoani Morogoro Maarufu kama FAMOGATA.

FAMOGATA ni kifupi cha maneno  Morogoro kuwa ghala la chakula nchini ni mpango ulioasisiwa mwaka 2006 na Rais Jakaya Kikiwete lebgo ni kuufanya mkoa wa Morogoro kuwa ndio mzalishaji mkuu wa chakula nchini.
Wakiongea na Mbiu ya Maendeleo katika maonesho ya sabasaba ya Mwalimu JK Nyerere maeneo ya nanenane mjini Morogoro, baadhi ya washiriki wamezitaka serikali na wadau wa kilimo kuhakikisha kuwa dhana ya Famogata inaendelezwa kwani dunia inakabiliwa na changamoto kubwa ya uzalishaji wa chakula kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vita, ukame n.k

No comments:

Post a Comment