Tuesday, September 30, 2014

FRANCIS Cheka kuzipiga na Mkenya Novemba 8


Francis Cheka akiwa na meneja wake Mohamed Kingoi

BONDIA bingwa wa ngumi za kulipwa nchini Francis Cheka Novemba 8 anataraji kushuka uwanja wa Jamuhuri Morogoro kuzichapa na Mkenya Daiel Wanyonyi ikiwa ni maandalizi ya kuutetea ubingwa wa WBO mwezi Desemba dhiidi ya Mwingereza Daniel Mstosh.


Meneja wa kampuni ya'Life Arts Production'inayodhamini pambano hilo Mohamed Kingoye na Mratibu wake Peter Kimathi walisema mbali na Mpambano huo kutakuwa na mapambano mengine matano likiwemo la Cosmas Cheka na Mkenya Fred Yekese.

"Kwanza Cheka bado ni bondia bora Afrika na Duniani kote akishikilia mikanda zaidi ya mitano, na mwezi Desemba anataraji kutetea mkanda mmoja na Mwingereza hivyo tumeamua kumtafutia pambano kumwimarisha"alisema Meneja Kingoye.

Kwa upande wao Francis na Cosmasi katika mazungumzo hayo na waandishi wa habari chama cha waandishi wa habari Moropc kwa nayakati tofauti walisema wamejiandaa kuonyesha burudani ya mwaka kutokana na kutonekana kwa muda mrefu lingoni.

"namfahamu Wanyonyi vizuri, nibondia mzuri ambae kwa uwezo wake mabiondia wengi nchini wanamkwepa kuzichapa naoe sasa nataka kuondoa hilo kwa kumtandika...kumbukeni najiandaa kuchapana na Mwingereza Mstosh"alisema Francis.

Alikili na mapromota kuwatelekeza mabondia kwa kutowatafutia michezo alisema imefika wakati wizara ya michezo kuangalia uwezekano wa kugharimia baadhi ya mampambano ikiwa ni hatua mojawapo ya kuongeza ajira kwa vijana.





No comments:

Post a Comment