Wednesday, September 3, 2014

UMASHUHURI wa Hamas waongezeka


Wafuasi wa Hamas
UMASHUHURI wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas umeongezeka huko katika eneo la Ukanda wa Ghaza lililoathiriwa na vita na katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, kufuatia mashambulizi ya siku 50 yaliyoanzishwa na Israel katika eneo hilo.

Kituo cha Sera na Utafiti cha Palestina kimetoa matokeo hayo ya uchunguzi wa maoni yaliyoonyesha kuwa, asilimia 61 ya Wapalestina wangemchagua Kiongozi wa Hamas Ismail Hania kama uchaguzi ungefanyika leo huko Ukanda wa Ghaza. Uchunguzi huo wa maoni umeonyesha pia kuwa, asilimia 32 ya Wapalestina wangemchagua Mahmoud Abbas Rais wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Palestina.
 Utafiti huo wa maoni uliofanywa miongoni mwa raia wa Palestina vile vile umeonyesha kuwa, asilimia 72 ya Wapalestina wanaunga mkono mapambano na harakati za muqawama dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel, kulinganisha na kile kinachojulikana kama mazungumzo ya amani na Israel yanayoungwa na chama cha Fat'h cha Mahmoud Abbas na nchi za Magharibi.
Uchunguzi huo wa maoni ulianza katika siku ya mwisho ya vita vya Israel huko Ghaza yaani tarehe 28 mwezi uliopita na kuendelea hadi katika siku za nne za mwanzo za usitishaji vita.  

No comments:

Post a Comment