Monday, July 28, 2014

LIBYA yaomba msaada wa kmataifa ili kuzima moto



SERIKALI ya Libya imeomba msaada wa kimataifa ilikuzima moto mkubwa unaoendelea kuchoma hifadhi ya mafuta mjini Tripoli baada ya makombora ya wapiganaji wa Kiislamu kulipua hifadhi ya takriban lita milioni 6 ya mafuta yaliyosafishwa.

Serikali hiyo changa inayoyumbishwa na mapigano baina ya makundi yanayopinga utawala uliomrithi Kiongozi wa miaka mingi Maummar Gaddaffi aliyeuawa katika mapinduzi ya 2011.
Pipa hilo ni moja ya maghala yanayomilikiwa na kampuni ya kitaifa ya mafuta nchini Libya - Brega
Msemaji wa kampuni hiyo Mohamed Al- Hariri anasema kuwa ikiwa moto huo utasambaa hadi kwenye mapipa mengine yaliyoko karibu basi itakuwa ni janga.
Serikli ya mpito nchini Libya imetaka kusitishwa mapigano ili kuruhusu wazima moto kuendelea na shughuli zao.




No comments:

Post a Comment