![]() |
| Shamba la mbegu ya mpunga la kampuni ya Tanseed ya mkoani Morogoro |
WAKULIMA
wilaya ya Mvomero,mkoani Morogoro
wameitaka Serikali, Mashirika na Taasi za utafiti nchini kuzalisha mbegu bora na
kuzitawanya kwa wakati kwa wakulima ili waweze kuzalisha kwa tija.
Wakizungumza na waandishi wa habari waliotembelea wilayani humo walisema endapo serikali itasimamia kikamilifu na kuwezesha upatikaji wa pembejeo taifa halitakumbwa na baa la njaa kama ilivyokuwa ikitokea miaka ya karibuni.
Aidha Hafeda Jonasi aliongeza kuwa mbali na serikali kutoa pembejeo kwa bei nafuu kwa wakulima kumekuwa na changamoto ya kuchelewa na kuchakachuliwa na watumishi wa serikali.
Mtafiti wa kutoka kituo cha kilimo
(mari)Mikocheni Dar es salaam Newton Temu alisema mpango wa taasisi hiyo ni
wakulima kutumia mbegu bora za kilimo zinazoletwa na watafiti kulingana na
maeneo.
Januari 2014
serikali kupitia wizara ya kilimo chakula na ushirika,kwa kushirikiana na
taasisi ya utafiti wa kilimo afrika (AATF) na tume ya sayansi na
teknolojia (costech) kupitia mradi wa water efficient maize for afrika na
wema-Tanzania walitambulisha mbegu mpya tatu za mahindi.

No comments:
Post a Comment