Saturday, July 26, 2014

TANESCO Kihansi yakiuka makubaliano na wanakijiji


Tanesco Kihansi, wilayani Kilombero, Morogoro

WANANCHI wa kijiji cha Mlimba A wilayani Kilombero wameligomea Shirika la Umeme nchini(TANESCO) tawi la Kihansi kutumia ardhi yao yenye ukubwa wa ekari 160 kwa madai ya kukiuka makubaliano baina yao.  


Tayari wananchi katika eneo wameaza kugawana kwa matumizi yao binafsi na shughuli za maendeleo baada ya kubaini kuwa shirika hilo lilitaka kuwatapeli na halina nia njema kwa mujibu wa makubaliano yao na shirika.

Mbele ya Afisa Tarafa ya Mliba Jordan Kisonga na kaimu meneja wa Tanesco tawi la Kihansi Idd Mangala kwenye mkutano kijijini hapo kusaka suluhu baina yao na shirika wanachi hao walisema muda wa kubembelezana na kuisotea haki yao umekwisha nakuwa sasa ni haki kabla ya wajibu.

Kwa mujibu wa wananchi hao akiwemo Jackline Gelvas na mwenyekiti wa kijiji Ramadhani Mkumba wabainisha kwa nia njema shirika hilo liliomba eneo hilo kwa ajili ya uwekezaji wa huduma za kijamii ikiwemo Hospitali na shule mwaka 1994 cha ni kuona wafanyakazi wa Tanesico kuonekana wakigawiana kinyemela.









No comments:

Post a Comment