Saturday, August 2, 2014

NAM , wafanya kikao kuzungumzia mapigano ya Israel


KIKAO  cha dharura cha kamati ya pamoja ya uratibu ya nchi wanachama wa harakati ya nchi zisizofungamana na siasa za upande wowote (NAM), kundi la 77 pamoja na China kimefanyika chini ya uwenyekiti wa Gholam-Hossein Dehqani, Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa.

 Kikao hicho cha dharura kimefanyika kufuatia kuendelea kwa mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya wananchi wasio na ulinzi wa Ukanda wa Ghaza sambamba na kuibuka maafa ya kibinadamu katika eneo hilo.
Iran imeitisha kikao hicho katika juhudi za kukomesha jinai za utawala wa Kizayuni huko Ghaza.

No comments:

Post a Comment