Thursday, August 7, 2014

UGONJWA wa Ebola waendelea kuuwa watu nchini Liberia


Waelimishaji kuhusu ugonjwa wa Ebola nchini Liberia

LIBERIA  imetangaza hatua za dharula dhidi ya ugonjwa wa Ebola kufuatia kasi kubwa ya kuenea kwa ugonjwa huo.

Rais wa Liberia Hellen Sirleaf amesema nchi yake kwa sasa inakabiliwa na tatizo la ugonjwa huo huku baadhi ya wananchi wakiwa na uelewa mdogo kuhusiana na hatua za kujikinga na ugonjwa huo.
Rais Sirleaf Johnson amelaumu ukosefu wa elimu na umaskini kama chanzo kikubwa cha maabukizi ya Ebola
Amesema baadhi ya shughuli za kijamii zimeahirishwa kwa muda ili kuepusha uwezekano wa watu kuambikizwa virusi vya Ebola.
Hatua hiyo ya Liberia inakuja huku wataalamu wa afya toka shirika la afya Ulimwenguni WHO wakikutana Geneva, Switzerland, kujadili mbinu za kukabiliana na ugonjwa huo.
Katika mkutano huo wa siku mbili wataalamu hao watajadili wautangaze ugonjwa wa Ebola kuwa janga la kidunia.










No comments:

Post a Comment