Thursday, August 7, 2014

MKUTANO wa marais wa Afrika na Obama wamalizika




Marais wa Afrika baadaya kumaliza kikao na Rais Obama
SIKU  tatu za mazungumzo yaliyolenga mustakabali wa bara la Afrika yamemalizika mjini Washington Marekani.

Mkutano huo ulikuwa wa kwanza wa aina yake kati ya Marekani na viongozi wa Afrika na ulilenga kuimarisha uhusiano kati ya Marekani na bara la Afrika.
Lakini kwa sasa mkutano umekamilika , nini kimefikiwa ? Nani amefaidika na kwa njia gani?
Viongozi wanajiandaa kundoka mjini humo na kwa mara nyingine kuongeza msongamano wa magari mjini DC.
Marais 40 wa Afrika walikwenda Marekani kuona kile ambacho Rais Obama alikuwa amewaitia katika jitihada zake za kuimarisha uhusiano kati ya Marekani na Afrika.
Waliondoka nchini humo wakiwa na mikataba ya uwekezaji ambapo makampuni ya Marekani yameahidi kuwekeza katika nchi zao.
Mikataba hiyo ni ya thamani ya dola bilioni 14 pamoja na ahadi ya Marekani kuimarisha uchumi na mataifa ya Afrika pamoja na mchango mwingine wa pesa ili kuimrisha miundo mbinu na upatikanaji wa kawin barani humo.






No comments:

Post a Comment