| Mkuu wa wilaya Kilombero Hassan Masala akipewa nishani |
DIWANI wa kata ya Mngeta kupitia chama cha
demokrasia na maendeleo(Chadema) Felisian Kigawa amemtunuku tuzo ya uongozi
uliotukuka Mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala kwa usimamizi bora
ulioharakisha maendeleo kata na tarafa ya Mngeta na wilaya hiyo kwa jumla.
Sambamba na
Dc.Masala wengine waliopata tuzo na vyeti ni pamoja na Padre Egfrid Tonz
alipata tuzo nne ikiwemo ya mchngo mkubwa wa maendeleo tarafani humo,kampuni ya
KP,Mkurugenzi mtendaji wa wilayani humo na Camfed walipata tuzo mojamoja.
Tuzo hizo
zilizotolewa mwishini mwa wiki zilikwenda sambamba na hafla ya uzinduzi
wa vyumba viwili vya maabara katika shule ya sekondari Kiburubutu
vilivyojengwa kwa hisani ya DEZA kupitia serikali ya Uswiss likiwa ni ombi la
Padri Tonz wa kanisa katoriki parokia ya Mchombe wilayani humo.
Kwa mujibu
wa diwani Kigawa wazo la tuzo kwa mkuu huyo wa wilaya linatokana na ombi la
wanachi kumpendekeza apate tuzo hiyo kutokana na kuthamini mchango wake kwa
wanachi hasa anavyotumia muda wake kukabili changamoto zinazo wakabili.
Kuhusu Padri Tonz, Kigawa alisema kwa muda mrefu amekuiwa chachu ya maendeleo yanyoonekana na kukua kwa kasi hasa ikizingatiwa amekuwa akiiwezesha tarafa hiyo kujikwamua na changamoto za kimsingi katika kuelekea kwenye maendeleo.
Kuhusu Padri Tonz, Kigawa alisema kwa muda mrefu amekuiwa chachu ya maendeleo yanyoonekana na kukua kwa kasi hasa ikizingatiwa amekuwa akiiwezesha tarafa hiyo kujikwamua na changamoto za kimsingi katika kuelekea kwenye maendeleo.
No comments:
Post a Comment