Tuesday, September 9, 2014

UJANGILI bado ni tishio nchini Tanzania


Asakari wa wanyma pori wakishuhudia ujangili wa wanyama
WAZIRI wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Lazaro Nyalandu  amesema kuwa, ujangili nchini humo bado unaendelea kushuhudiwa licha ya kuweko juhudi za kupambana nao.

Amesema hayo mjini Dar es Salaam katika mkutano wa wadau wa maendeleo ya kupambana na ujangili na kusisitiza kwamba, kunaendelea kufanyika juhudi za kubuni mbinu ili kukomesha vitendo hivyo.
Waziri Nyalandu amesema mkutano huo ni mwendelezo wa mkutano uliofanyika Mei mwaka huu ukilenga kuwasilisha utekelezaji wa makubaliano waliyoafikiana kila taifa ili kuona namna gani watasonga mbele katika kukabiliana na viendo vya ujangili.
Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa, moja ya hatua walizochukua ili kupambana na vitendo vya ujangili katika mbunga za wanyama ni kuajiri askari wanyamapori 430 na hadi Septemba mwaka huu wamelenga kupata askari 900.

No comments:

Post a Comment