![]() |
| Wachezaji wa ngoma ya jadi nchini Misri |
BODI ya kidini
ya misri, imetoa fatwa kukataza uonyeshaji wa kipindi kilichoanzishwa kwenye
televesheni nchini humo kuonyesha densi ya jadi ya wanawake wa misri ya
kunengua viuno almaarufu 'belly dance'.
Ngoma hiyo inayofanana na chakacha
ya waswahili imechezwa tangu zama za kale na imenakiliwa hata katika enzi za
ma-pharoah katika nchi hiyo ya Misri.
Ni densi ambayo isingekosekana
kwenye sherehe muhimu. Harusi au burudani nyenginezo.
Maelfu ya watalii wanaoitembelea
Misri hupenda kwenda kuona inavyochezwa lakini mnamo siku za hivi karibuni
wasichana kutoka sehemu nyingi duniani hasa ulaya na hata uchina wameripotiwa
kwenda Misri kujifundisha jinsi ya kucheza densi hiyo.
Ni ajabu kuwa sasa imekuwa maarufu
katika mataifa ya kigeni kuliko Misri kwenyewe ambako haichezwi ovyo ovyo
hadharani.

No comments:
Post a Comment