Wednesday, September 3, 2014

NIGERIA kuishitaki klabu ya Schalke ya Ujerumani


Chinedu Obasi
SHIRIKISHO  la soka Nigeria limesesema litaishitaki klabu ya Schalke ya Ujerumani kwa Fifa baada ya klabu hiyo kukataa kumruhusu mshambulizi Chinedu Obasi kushirki michuano ya kufuzu kombe la mataifa ya Afrika mwaka 2015.

Hata hivyo klabu ya Schalke imesema kuwa sababu ya kukosa kumruhusu mchezaji huyo kuondoka ni kwamba pasi yake ya usafiri iko katika ubalozi huku viza yake ikitayarishwa kabla ya kuanza kwa michunao ya klabu bingwa Ulaya.
Nigeria ambao ni mabingwa wa Afrika, watamenyana na Congo mnamo tarehe sita Septemba.
Siku nne baadaye watatoana kijasho na Afrika Kusini. Nigeria imekasirishwa na
Schalke kuhusu mchezaji wake Obasi.

No comments:

Post a Comment