Wednesday, September 17, 2014

WAZIRI WA nje wa Iran awasili Newyork



Waziri wa mambo ya nje wa Iran (katikati)akiwasili Newyork Marekani

MUHAMMAD  JAVAD  ZARIFU, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amewasili mjini New York kwa minajili ya kushiriki kwenye mkutano wa 69 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na katika duru mpya ya mazungumzo kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kundi la 5+1. 

Katika safari yake hiyo huko New York, Muhammad Javad Zarif ameongozana na Abbas Araqchi Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayehusika na masuala ya kimataifa, Majid Takhte Ravanchi, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayehusika na masuala ya Ulaya na Marekani, Hamid Baid Nejad, Mkurugenzi wa masuala ya kisiasa na kimataifa na maafisa wengine wa kisiasa, kisheria na vyombo vya habari wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran. 
Duru ya saba ya mazungumzo kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na nchi wanachama wa kundi la 5+1 itafanyika kesho Alhamisi katika ngazi ya Manaibu Mawaziri wa Mambo ya Nje. Muhammad Javad Zarif Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran na bi Catherine Ashton Mkuu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya pia watashiriki kwenye mazungumzo hayo ya New York.

No comments:

Post a Comment