Saturday, August 15, 2015

EKARI 100 zatengwa kwaajili ya mkoa mpya wa Ulanga


Watumishi wa Halmashauri ya Kilombero

HALMASHAURI ya wilaya ya Kilombero imeanza maandalizi ya ujenzi wa makao makuu ya Mkoa mpya wa Ulanga kwa kutenga eneo ekari 100
.

Maandalizi hayo yamefahamika katika kikao cha kamati ya ushauri ya wilaya(DCC)mjini Ifakara wakati mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero Azimina Mbilinyi akiwasilisha hoja ya ya kuugawa mkoa wa Morogoro zilimo wilaya ya Ulanga na Kilombero ili kusogeza huduma za kijamii na maendeleo karibu na wananchi.

Mbele ya mwenyekiti na kaimu mkuu wa wilaya ya Kilombero ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Ulanga Christina Mdeme, Mkurugenzi Azimina alisema uamuzi huo ulijumuisha eneo linalopakana na kijiji cha Kapolo,Kikwawila,Lungongole na Katindiuka unakuaja baada ya kuamuliwa makao makuu ya mkoa huo mpya kuwa wilayani Kilombero.

"Eneo hili litahusisha ujenzi wa Ikulu ndogo na usalama wa Taifa ekari 50 kati,ekari 30 ujenzi wa ofisi za uhamiaji,takukuru,mahakama na polisi na ekari 20 zitakuwa akiba kwa ajili ya ujenzi wa taasisi nyingine za serikali kwa kadri itakavyohitajika"Alifafanua Azimina.

Alisema alisema ombi la moka wa morogoro kugawanywa lilitokana na mkoa huo kuwa mkubwa, changamoto ya jiografia yake, changamoto ya upatikanaji huduma za maendeleo na ufanisi wake katika utawala na usimamizi wa shughuli za maendeleo.

"amkoa huu utakaokuwa  na ukubwa wa Kilomita za eneo 39.4 utakuwa na watu 673,080 ukigawanyika katika wilaya tatu ikiwemo ya Ulanga,Kilombero na Malinyi halmashauri nne ikiwemo ya Ulanga,Malinyi,Kilombero na halmashauri ya mji wa Ifakara na majimbo manne"alisema Mkurugenzi huyo.

kwa mujibu wa mkurugenzi huyo fursa za wilaya hizo na mkoa zitakuwa ni ardhi,jiografia,miundombinu,uchumi na huduma za kijamii akifafanua kuwa wilaya ina kilomita za mraba 14,918 na watu 407,880 wenye kaya 94,604. 

Akipongeza mpango mkakati huo kaimu mkuu wa wilaya hiyo Christina,aliwapongeza  wajumbe kwa kupitisha kwa kauli moja ya kufanya Ifakara kuwa makao makuu ya mkoa mpya na kusema mkoa mpya umekidhi vigezo vyote vya kutakiwa kuwa mkoa isipokuwa kigezo kimoja cha kuwa na tarafa chache.

Christina  alisema mkoa utakuwa na kata 66,vijijiji 202,kilomita za mraba 39,483 na watu 673,080 na tarafa 12 na kusema lengo la kugawa mkoa ni kusogeza huduma kwa wananchi na kuwaletea karibu maendeleo yao.
Ifakara kuwa makao makuu ya mkoa mpya na kusema mkoa mpya umekidhi vigezo vyote vya kutakiwa kuwa mkoa isipokuwa kigezo kimoja cha kuwa na tarafa chache.

Christina  alisema mkoa utakuwa na kata 66,vijijiji 202,kilomita za mraba 39,483 na watu 673,080 na tarafa 12 na kusema lengo la kugawa mkoa ni kusogeza huduma kwa wananchi na kuwaletea karibu maendeleo yao

No comments:

Post a Comment