Saturday, August 15, 2015

FOMU za Ubunge Morogoro zaanza kuchukuliwa


Mwenyekti wa H/w Kilosa aliyesimama kati akiwa na wanafunzi

WAKATI zoezi la uchuakuaji fomu za kuwania ubunge kutoka Tume ya Taifa zikianza kutolewa nchi nzima,jana juzi mitaa ya kilosa kati ilifungwa kwa muda wakati mgombea ubunge Abeid Malapakolo kupitia Ukawa akiwakilisha chama cha wanachi CUF alipokwenda kuchukua fomu katika ofisi za Halmashauri hiyo.


Mkoa wa Morogoro una jumla ya majimbo 11 kati ya hayo majimbo tisa wagombea wake watakuwa ni wa chama Demokrasia na Maendeleo Chadema kupitia Ukawa na majimbo mawili likiwemo la Kilosa na Morogoro kusini watawakilishwa na wagombea kutoka Cuf.

Mara baada ya kuchukuwa fomu Mlapakolo alisema umati huo unatokana na watanzania kukubali mabadiliko chini ya mwamvuli wa ukawa nakuwa lengo lao si polojo bali maendeleo ya kweli dhiidi ya umasikini unaowakabili sasa.

“Mwalimu Nyerere alisema watanzania wanahitaji mabadiliko wasipoyapata ndani ya CCM watayapata nje ya CCM sasa umefika muda wa watanazina kuhitaji mabadiliko ambayo bila shaka yoyote yatatimia mwaka huu”alisema Mlapakolo.

Alisema kuwa kama atafanikiwa kuwa mbunge wa jimbo la Kilosa atahakikisa kuwa migogoro ya ardhi dhidi ya wakulima na wafugaji  iliyodumu kwa muda mrefu atahakikisha inapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Wilaya ya Kilosa ina majimbo mawili ya Mikumi na Kilosa kati ambapo jimbo la mikumi litawakishwa na Joseph Haule(Profesa Jey)Chadema na Kilosa Abed Mlapakolo wote wanatokana na umoja wa vyama vilivyoungana vya Ukawa.

Mlapakolo atachuana vikali na wenzeke kaadhaa katika kinyang’anyilo hicho kama vile  Hemed Limano wa Democratic Party na Mbaraka Bawaziri wa CCM ambapo alisema wananchi wanakila sababu ya kumchagua yeye kwa maendeleo zaidi kwa wana kilosa.

Idd Abdurrahman ni msimamizi wa uchaguzi katika wilaya ya Kilosa amewataka wagombea wate kuwapa elimu wapenzi na wanachama wao kutofanya fujo wakati wa kampeni na hata siku ya kupiga kura kwani uchaguzi utakuwa wa uhuru na haki.


No comments:

Post a Comment