Wednesday, September 2, 2015

ASILIMIA 50 ya wanawake dunia kumiliki utajiri ifikapo mwaka 2016


Prof Amina mama 
LICHA ya dunia kukabiliwa na majanga mbalimbali likiwemo la njaa, takwimu zinaonyesha ifikapo mwaka 2016 asilimia 50 ya wanawake duniani watakuwa wanamiliki utajiri uliopo katika jamii.


Hayo yalisemwa  jijini  Dar es Salaam jana na  mwanaharakati wa haki za wanawake  kutoka  nchini  Nigeria Profesa  Amina Mama wakati wa tamasha la Mtandao wa Jinsia Tanzania  (TGNP).

Profesa Mama  alisema uchambuzi wa Kifeministi unaonyesha hakuna uhuru  wowote katika sera za soko huria zilizoletwa na taasisi za kifedha hali iliyosababisha matabaka na pengo la walionacho na wasionacho hususani wanawake.

"Tunatambua kuwa wanawake wamekuwa wakifanya kazi nyingi kwa muda mrefu katika mazingira magumu na kuwasababishia msongo wa mawazo ili tu kukidhi mahitaji yao...inachochea pia umasikini dhiidi yao lakini sasa wanaamka kwa kasi kubwa kama ilivyo nchini Naijeria"alisema Profesa Mama.

 Akiwasihi kuhakikisha wanafanikisha mabadiliko ya kiukombozi ilikujenga usawa dhiidi wanawake lazima wahoji na kuchambua kwa kina  sera za viongozi  wanaoingia madarakani madarakani.

"mfano wa nchi katika mataifa ya magharibi wanawake wenye kazi maofisini  wanapoenda kazini huwa waacha walezi wa watoto wao majumbani"aliongeza.

Alisema kwa sasa kuna ongezeko  kubwa la watoto ambao hawalelewi na wazazi wao, wazazi wako bize na kutafuta pesa hivyo kuhoji nchi imepiga hatua gani tangu enzi za utumwa.


Kwa mujibu wa Profesa Mama harakati za Kifeminsiti zimejikita katika mzizi na kuleta uhai,yaani mabadiliko ambayo yanalenga kugusa tatizo ambalo linaweza kuwa si moja isipokuwa muunganiko wa masuala mengi ya k

No comments:

Post a Comment