Nyaya
zote nne zinazopeleka umeme katika jimbo hilo la Crimea zimekatwa sasa na
kuwaacha wakaazi zaidi ya milioni mbili bila umeme.
Picha
zilizosambazwa kupitia mitandao ya kijamii zinaonesha nyaya za umeme zikiwa
zimetundikwa bendera ya Ukraine.
Crimea
ilimegwa kutoka Ukraine na Urusi mwaka uliopita lakini utawala nchini Ukraine
umekuwa ukipeleka umeme eneo hilo.
Viongozi
wa jimbo hilo wanasema kuwa wamejaribu kurejesha umeme katika miji ya
Simferopol, Yalta na Saky wakitumia generata lakini hautoshi.
Kwa
mujibu wa naibu waziri wa Crimea, Mikhail Sheremet, hospitali na zahanati
zingine za afya ndizo zilizopewa kipaombele.

No comments:
Post a Comment