Sunday, November 22, 2015

MILIPUKO yatikisa Iraq

MILIPUKO  kadhaa imeutikisa mji mkuu wa Iraq Baghdad na taarifa za awali zinasema kuwa, watu wasiopungua 10 wamepoteza maisha yao.


Vyombo vya usalama na duru za hospitali zinasema kuwa, kwa uchache watu 10 wamepoteza maisha yao na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia milipuko tofauti na ufyatuaji risasi uliotokea mjini Baghdad na katika viunga vya mji huo. Polisi ya Baghdad imetangaza kuwa, mlipuko wa kwanza ulitokea katika soko moja mjini humo katika eneo la al-Forat. Aidha vyombo vya usalama vya Baghdad vinasema kuwa, katika tukio jingine, watu wasiojulikana wakiwa na silaha wameshambulia kituo kimoja cha upekuzi katika mji wa Yusufiya uliopo umbali wa kilomita 40 kutoka katika mji mkuu huo. Wakati huo huo jana kulitokea mlipuko wa bomu la kutegwa barabarani katika eneo la Hur lililoko kusini mwa Baghdad na kupelekea kuuawa polisi mmoja.

No comments:

Post a Comment