Friday, November 27, 2015

KARANTINI ya ugonjwa wa kipindupindu yaondolewa Ulanga

Halmashauri ya wilaya Ulanga 
KARANTINI iliyokuwa imewekwa na idara Afya tarafa ya Mwaya wilayani Ulanga kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu uliolipuka mapema mwezi huu na kusababisha zaidi watu 70 kukumbwa na ugonjwa huo imeondolewa baada ya ugonjwa huo kudhibitiwa.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake,Mganga wa kituo cha Afya Mwaya wilayani humo Dk Amos Mlai alisema ugonjwa huo uliokuwa umelipuka mwanzoni wa mwezi huu ulisababisha karibu watu 50 kukumbwa na ugonjwa huo na kuwa tishio katika vijiji vinavyoizunguka tarafa hiyo. 

"historia ya ugonjwa huu uliletwa ma mama mmoja kutoka jijini Dar es salaam aliyekuwa amekuja kwenye sherehe za kimila,alipofika jioni alinza kujisikia vibaya kisha kutapika na kuharisha mfululizo...akawahi tiba hapa kituoni lakini baada ya siku kadhaa wakaanza kuletwa watu wengine mfululizo toka vijiji vya jirani"alisema Dk Mlai.

Dk Mlai alifafanua kuwa uchunguzi ulibaini vifaa alivyokuwa akitumia mgonjwa wa awali vilitumika bila tahadhali na watu wengine sambamba na nguo zake kufuliwa kwenye mto ambao maji yake hutumika kwa shughuli za kila siku majumbani na wanachi wa vijiji vya jiarani.

"tukaamua kuviweka karantini vijiji vile na kuanza kutoa elimu ya afya ikiwemo kuoacha kabisa kusalimiana kwa kushikana na mikono,kufunga vyakula vinavyouzwa sambamba na pombe za kienyeji lakini pia kuzuia uingiaji na utokaji wa mtu yeyote kijiji humo...kwa kuda wa siku tano hivi hali ile ikawa miedhibitika"alisema dk Mlai.



No comments:

Post a Comment