Thursday, November 19, 2015

MAJALIWA aidhinishwa na Bunge kuwa waziri mkuu wa Tanzania

Majaliwa K. Majaliwa
MBUNGE  wa Ruangwa Majaliwa Kassim Majaliwa ameidhinishwa na Bunge la Tanzania kuwa waziri mkuu mpya wa Tanzania.


Bw Majaliwa amepata kura 258 kati ya 351 zilizopigwa, baada ya Spika wa Bunge Job Ndugai kutangazia bunge kwamba ndiye aliyekuwa amependekezwa na Rais John Pombe Magufuli awe Waziri Mkuu.

Bw Majaliwa, 55, amekuwa mbunge wa jimbo la Ruangwa, Jimbo la Lindi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) tangu 2010.


No comments:

Post a Comment