|
MTANDAO wa mashirika
yanayotetea usawa wa kijinsia na haki za binadamu(FEMACT) na wanaharakati wa
demokrasia na maendeleo ngazi ya jamii (GDSS) wamemkubusha Rais Dk.John
Magufuli kuzingatia usawa wa kijinsia kwa kuwakumbuka wananwake kwenye muundo
wa serikali yake ya awamu ya tano.
Hayo yamo kwenye
majumuisho na makubaliano ya asasi hizo yaliyotolewa kwa nyakati tofauti
baada ya semina ya uboreshaji mapambano dhiidi ya unyanyasaji wa kijisinsia
kupitia mikataba ya kiamatifa.
Tamko lililotolewa na
viongozi mbalimbali wa asasi,mashirika na mitandao akiwemo Mwenyekiti –
FemAct Abdullah Othman, Mkurugenzi mtendaji wa mtandao wa jinsia TGNP Lilian
Liundi, na Mwakilishi wa mafunzo ya jinsia na Maendeleo Seleman Bishagazi
walimshauri Rais kuikumbuka mikataba hiyo wakati akiunda serikali.
Kwa mujibu wa
viongozio baadhi ya mikataba iliyoridhiwa ni pamoja na Tamko la Umoja wa
Matifa la Haki za Binadamu(UDHR:1948), Mkataba wa Kimataifa wa Kutokomeza
Ubaguzi dhidi ya Wanawake (CEDAW: 1979, Articles 7: a, b na c), Mpango Kazi
wa Beijing (1995), Mkataba wa Ziada wa Maputo, na Mkataba wa Nyongeza wa
jinsia na Maendeleo kusini mwa Africa (SADC Gender Protocol,).
“Rais ameanza na
uteuzi wa baraza la mawaziri,tulitarajia uteuzi huo kufikia 50 kwa 50 lakini
katika uteuzi alioufanya tumeshuhudia wanake ni karibu asilimia 27 yaani
imeshuka ikilinganishwa na seriakli iliyopita… tunaomba kunga mkono makatamko
hayo katika teuzi zijazo”alifafanua Abdullah Othman na kuongeza
“tunaendelea kuhimiza
usawa wa kijinsia katika teuzi zijazo kama Wabunge, Wakuu wa Mikoa na wilaya,
Makatibu Tawala wa Mikoa na wilaya,Makatibu Wakuu na Naibu wao wizarani,
Wakurugenzi,Wakuu wa taasisi na makampuni, mashirika ya umma na bodi zake
bila kuusahau mhimili wa mahakama”
|
No comments:
Post a Comment