Thursday, December 17, 2015

WAKULIMA wa miwa bonde la Kilombero walia na rushwa



WAKULIMA wa miwa bonde la Ruhembe  wilayani Kilombero,mkoa waMorogoro  wamesema wamechoshwa na wizi unaoambatana na rushwa katika viwanda vya sukari Illovo na kuwataka wabunge wa Chadema jimbo la Mikumi-Kilosa Joseph Haule‘Profesa Jey’,jimbo la Ifakara-Kilombero Peter Lijualikali na Devotha Minja wa viti maalum kumwita kwa siri Rais John Magufuli na waziri mkuu Majaliwa Kasim kuwasafisha wezi hao.

Mbele ya wabungea hao waliamua kuunda timu ya mafanikio itakayozikabili changamoto zinazowabaili wananchi mkoani Morogoro wakiwemo wakulima hao baadhi yao Mohamed Kapyela na Rukia Kahuka walisema uongozi wa viwanda vya sukari ILLOVO  K1 na K2 na viongozi wa vyama vya ushirika wanashirikiana na kuwapunja malipo yao.
“kama huna kati ya 100,000 hadi 200,000 kuhonga makarai wa mizani getini lazima uibiwe kilo na kiasi cha sukari kwenye maabara zao,ajabu ni miwa yetu pekee ambayo ni myepesi na haina sukari lakini miwa ya kiwanda ni mizito na inasukari nyingi…jamani mwiteni Rais Dk John Magufuli aje na huku”alsema Kahuka.
Mbele ya wabunge hao walisema mbali na wizi huo bado hakuna ratiba inayoeleweka ya uvunaji miwa kwa wakulima wanje,hakuna uwiano wa uingizaji miwa kindani,kuna mapunjo katika kutambua kiasi cha sukari kwenye mua katika maabala kiwandani hapo na hata malipo hayatoki kama inavyotarajiwa kwa kurundikiwa makato yasiyoeleweka.
Mohamed Kapyela alisema viongozi hao wanashirikiana na uongozi wa kiwanda kupunguza kiasi cha miwa kutoka nje kusindikwa kiwandani hapo na kusbabisha miwa mingi ya wakulima wa nje kulala hadi zaidi ya miaka miwili bila kusindikwa na wakulima kukosa pato la kujikimu.
Aidha walisema vyama vikubwa kikiwemo cha RCGA na KCGA amegeuka vinara kwa kukiuka katiba na  kuzibadili ili waongoze milele na wamekuwa wakitumia ukubwa wavyama hivyo kuwakandamiza wakulima wadogo na vyama vidogo kwa kuzuia miwa isiingie kiwandani hivyo zaidi ya tani 600 kutupwa kila mwaka bila kujali hasara.
Kutokana na vilio hivyo wabunge hao waliazimia kupeleka hoja binafsi ya kuvilejesha serikalini viwanada vilivyokiuka mikataba katika bunge lijalo mwezi januari Mwakani sambamba na kumtaka waziri mkuu kufika kiwandani hapo haraka kuwashugulikia viongozi 'miungu watu' kwenye vyama kikiwemo cha Ruhembe Cane growers association-RCGA.
Mbunge Lijualikali na Devotha kwa nyakati tofauti walipinga unyanyasaji wanaofanyiwa wakulima hao wakiahidi kuwalinda na kuwatetea hadi hatua ya mwisho ikiwemo kurejeshewa mapunjo ambayo wamekuwa wakifanyiwa kwa kipindi kilichopita.
RAIS wa Tanzania John Pombe Magufuli amewahak

No comments:

Post a Comment