Monday, June 16, 2014

MKUU wa mkoa Morogoro ampa mwezi mmoja mwenyekiti na mkurugenzi wa Halmashauri ya Morogoro kujibu madai ya kamati ya bunge




 
Mkuu wa mkoa wa Morogoro akizungumza na waandishi wa habari mjini Morogoro
MKUU wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera amempa mwezi mmoja mwenyekiti na Mkurugenzi wa Halmashuri ya Morogoro kujibu madai yote yaliyotolewa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za serikali za Mitaa (LAAC)dhiidi ya halmashauri hiyo.


Agizo la Bendera kwenye baraza la madiwani mwishoni mwa wiki linakuja baada ya ukaguzi kamati ya bunge mwaka 2013 na mkaguzi wa hesabu za serikali CAG 2012/13 kubaini mapungufu mengi katika matumizi ya fedha za umma.
 
Akionyesha kupuuzwa kwa maagizi ya CAG na LAAC, Bendera alisema mkoa hautakubaliana na dosari kama hizo za kiutendaji katika mkoa huo.

kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Kibena Kingu  alimhakikishia  mkuu huyo wa mkoa kuwa  halmashauri yake imejipanga ipasavyo kuhakikisha hoja hizo sugu zinashughulikiwa.

Kibena  alimweleza Bendera kuwa ili kutekeleza kwa vitendo changamoto hizo halamashauri imejipanga kukusanya kodi kwa zaidi ya asilimia 50 kotoka asilimia 37 mwaka 2013/2014.

Mbali na hilo pia aliongeza kuwa halmashauri imeamua kudhjibiti mianya ya uvujaji fedha za umma kwa kufuarta maelekezo ya CAG na kuhakikisha tham,ani ya fedha inakweda sambamba na kusudio katika utekelezaji.



















No comments:

Post a Comment