Monday, June 16, 2014

WIZARA ya mambo ya ndani yajibu ya rushwa dhidi ya usaili wa uhamiaji



WIZARA ya mambo ya ndani ya nchi imesema tuhuma za rushwa zinazohambatanishwa na kazi ya usaili na nafasi ya mkaguzi msaidizi wa uhamiaji ni hisia tu za wahusika
.

Taarifa ya msemaji wa wizara hiyo  Isaac Nantanga inasema kuwepo kwa tuhuma za kuwepo kwa rushwa wakati wa kazi za usaili ni hisia na hazina ushahidi na kuwa usaili ulifanywa kwa kufuata kanuni na sheria zinazosimamia ajira za utumishi wa umma .

Nantanga amesema waombaji zaidi walitumia haki yao ya msingi kuomba nafasi hizo na kutokana na wingi huo wizara ilifanya mchujo wa awali na kubakiwa na maombi 10,500 ya watu wenye sifa .

Amesema wizara ilitambua haki ya kila muombaji ya kupatiwa nafasi ya kushindaniwa nafasi hizo ikabidi ifanyike utaratibu wa kutafuta eneo lenye nafasi kwa ajili ya usaili huo

No comments:

Post a Comment