Monday, June 16, 2014

MAADHIMISHO ya wiki ya utumishi wa umma yafunguliwa leo jijini Dar



 
Waziri ofisi ya Raisi utawala bora kapteini George Mkuchika akiongea  viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar

MAADHIMISHO ya wiki ya utumishi wa umma yamefunguliwa leo katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam na waziri wa nchi ofisi ya Raisi (Utawala bora) Kapteni mstaafu George Mkuchika ambapo amewataka watanzania kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayokujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na baadhi ya wizara na Taasisi zake.


Maadhimishohayo yanatarajiwa kumalizika juni 23 ambapo yatafungwa kwa kutolewa hotuba mbalimbali toka kwa viongozi wa serikali.

Kauli mbiu ya mwaka hu ya maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma ni mkataba wa msingi na kanuni za utumishi wa umma barani Afrika ni chachu ya kuimarisha utawala bora na uendeshaji wa shughuli za serikali kwa uwazi.  

No comments:

Post a Comment