Tuesday, July 8, 2014

ANUSURIKA kufa bada ya kujeruhiwa kwa panga


Wauguzi hospitali ya Morogoro

MWANAMKE Faustina Sezali(38)wa kijiji cha Lukuyu Tarafa ya Mgeta wilayani Mvomero amenusurika kufa baada ya kujeruhiwa kwa panga na mtu anayedaiwa kuwa ni mume wake kwa ajili ya ugomvi wa kugombea mali.


Faustina akizungumza kwa taabu katika hospitali ya rufaa mkoani Morogoro alipolazwa akiugulia majeraha mbalimbali za mwili wake ikiwemo kichwani na mgongoni alimtaja aliyemjeruhi wakigombea mali kuwa ni Rogasiani Jeremiasi.


Mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro Dr.Ritta Lyamuya ameeleza kuwa hali ya majeruhi inaendelea vema baada ya kupata huduma ya kwanza.

Hata hivyuo jeshi la polisi limekili kupata taarifa ya Mwanamke huyo nakuwa anaendelea na matibabu katika hoispitali hiyo wakati jeshi linamsak mtuhumiwa wa tukio hilo.




No comments:

Post a Comment