Tuesday, July 8, 2014

BEI ya vyakula soko la Mabibo yashuka



 
Wafanyabiashara wa ndizi soko la Mabibo ,Dar
 BEI ya vyakula katika soko la ndizi la Mabibo imeendelea kushuka na kutoongezeka 
kwa muda mrefu sasa toka kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Wakiongea na Mbiu ya Maendeleo mapema leo subuhi katika soko la Mabibo lililopo , Manispa ya Kinondoni jijini Dar es salaam ,baadhi ya wanunuzi na wafanyabiashara walimweleza mwandishi kuwa hali imetokana na uzalishaji wa mazao toka mikoa kuongeza kwa mwaka huu.

Kwa upande wao wananchi wanaopta huduma ya kununua vyakula mbalimbali toka sokoni hapo wameshukuru kwani imechangia bei ya futari katika mikahawa na mamama na babalishe katika maeneo mbalimbali ya jiji kupungua.

No comments:

Post a Comment