Friday, July 11, 2014

KJIJI cha Pandaguo, Lamu nchini Kenya chavamiwa



WATU  300 waliokuwa wamejihami wamevamia kijiji cha Pandanguo katika Kaunti ya Lamu Pwani ya Kenya.

Chifu wa eneo hilo Karisa Charo Karisa, anasema kuwa shule na nyumba nne ziliteketezwa katika mashambulizi hayo yaliyofanywa usiku wa kuamkia leo ikiwemo shule moja ya msingi.
Duru zinaarifu kuwa washambuliaji hao walifanya uvamizi saa tatu usiku na kuiba bunduki sita kutoka kwa polisi wa akiba.
Walivamia msikiti ambako polisi hao wa akiba walikuwa wanasali. Mmoja wa polisi hao aliyeponea kifo aliambia waandishi wa habari kuwa  waliambiwa wachague kati ya mauti na bunduki zao.
Mnamo mwezi Juni watu watano waliuawa katika eneo hilo la Pandanguo ambalo liko umbali wa kilomita 30 kutoka Mpeketoni ambako mashambulizi mengine yaliwaacha watu zaidi ya sitini wakiwa wameuawa.
Mashambulizi ya Kwanza yaliyofanyika mjini Mpeketoni, yalisemekana kufanywa na kundi la wanamgambo la Al Shabaab ingawa serikali alilalaumu wanasiasa kuyachochea mashambulizi hayo.




No comments:

Post a Comment