Friday, July 11, 2014

WAKULIMA wa vitunguu Kilolo walia na ubovu wa miundo mbinu


Mkulima wa vitunguu akiandaa shamba

WAKULIMA wa zao la kitunguu katika vijiji vya Msosa na Mtandika  wilayani Kilolo mkoa wa Iringa , wanakabiliwa na changamoto ya miundo mbinu ya kisasa ya umwagiliaji
.
Wakiongea na mwandishi wa mbiu ya Maendeleo katika vijiji hivyo hivi karibuni , baadhi ya wakulima wamesema kuwa, msimu wa uandaaji wa mashamba ya kwaajili ya kilimo cha vitunguu umeanza lakini hali ya miundo mbinu yaumwagiliaji imechakaa kiasi cha kusababisha kushuka kwa uzalishaji  wa zao hilo.
Wamesema miundo mbinu ya umwagiliaji katika eneo hilo imeharibiwa na mvua za masika zilizopita hivyo ni vyema wadau na serikali kuwasaidia kuboresha ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo.

No comments:

Post a Comment