Wednesday, July 9, 2014

MWENYEJI wa michuano ya kombe la dunia apigwa wiki



MWENYEJI  wa michuano ya soka ya Kombe la Dunia la mpira wa miguu, Brazil ametolewa na Ujerumani katika mechi ya nusu fainali iliyofanyika jana baada ya kufungwa mabao 7 kwa 1 katika uwanja wa Mineirao.

Ujerumani ilianza kuongoza kwa bao la kwanza lililofungwa na Thomas Muller katika dakika ya 11 baada ya kupigiwa mpira wa kona kutoka upande wa kulia.

Goli la Muller lilifuatiwa na goli la pili lililofungwa na mchezaji mwenzake Miroslav Klose katika dakika ya 23. Akizungumzia mechi hiyo kocha wa Ujerumani Joachim Loew amesema kuwa, mwenyeji Brazil alishindwa kukabiliana na mashambulizi ya kila upande ya Ujerumani.
Sasa timu ya Taifa ya Ujerumani itakutana Jumapili ijayo katika fainali ya kombe la dunia na mshindi wa nusu fainali kati ya Argentina na Uholanzi.

















No comments:

Post a Comment