Thursday, July 10, 2014

MWENYEKITI Halmashauri awaagiza viongozi wa vijiji kuwaondoa wafugaji wavamizi



 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kilosa Ameir Mubaraka
MWENYEKITI wa halmashauri ya wilaya ya Kilosa Ameir Mubaraka Nahdi amewaagiza viongozi wa vijiji vya kata Lumuma wilayani  humo kutumia kipindi hiki cha kiangazi kuwaondoa wafugaji wote wavamizi wa maeneo ya wakulima. 


Agizo hilo alilitoa kitongojini Manyomvi katika sherehe ya mkulima iliyoandaliwa na mradi wa mpango wa kupunguza hewa ukaa inayotokana na uharibifu na ufyekaji ovyo wa misitu MKUHUMI chini ya shirika la kuifadhi misitu ya asili Tanzania TFCG.

Kwa mujibu wa Mubaruk serikali wilayani humo imechoshwa na kelele baina ya wakulima na wafugaji ambazo kwa muda mrefu zimeiweka wilaya hiyo kwenye ramani ya machafuko ya migogoro ya ardhi kwa muda mrefu.

Awali afisa kilimo wa mradi wa mkuhumi Shadrack Nyungwa alieleza lengo la maadhimisho ya sherehe hiyo ni kupongezana na kupeana zawadi na kuhamasisha jamii kuongeza bidii ya utunzaji mazingira shambani.

Vijiji 8  vimeshiriki na kupatiwa mafunzo ya kilimo hifadhi na mazingira ambavyo ni Manyomvi,mlenga,Idete  na Mfuluni, vingine ni Kisongwe, Lunenzi, Ibingu na chabima.









No comments:

Post a Comment