Thursday, July 10, 2014

WATANZANIA washauriwa kuwatunza watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi


Wanawake wa  Mazimbu Morogoro

WATANZANIA wameshauriwa kuliangalia kundi la watoto wanaozaliwa kwenye mazingira hatarishi,wakiwa na upungufu wa akili badala ya kuwanyanyapaa na kuwatelekeza kama inavyojitokeza katika maeneo mbalimbali nchini.


Baadhi ya wanawake wa Mkoani Morogoro walisema hayo wakati wakizungumza walipotembelea kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu na walio na upungufu wa akili cha Mehayo, kilichopo Mazimbu Mkoani Morogoro.

Mmoja wa wanawake hao, Elizabeth Mtambo, ambaye pia ni makamu Mwenyekiti wa Kikundi cha wanawake cha Kizota, kutoka chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA, alisema tabia ya baadhi ya wazazi na walezi kuwatelekeza watoto wenye matatizo ya akili na waishio katika mazingira magumu,imesababishwa na ukosefu wa elimu ya kutosha kuhusu umuhimu wa watoto hao, na kulaani baadhi ya wanawake wanaoshiriki ukatili huo.

Aidha Mlezi wa kituo cha Mehayo, Prisca Chinyama, aliishauri Serikali katika kukabiliana na hali hiyo, ni vyema wakaangalia uwezekano wa kutunga sheria kali ili kuwabana watakaobainika kuwanyanyasa watoto wenye matatizo ya akili na walio katika mazingira magumu.

No comments:

Post a Comment