Wednesday, July 9, 2014

VIKOSI vya serikali vyafanikiwa kuidhibiti Ikulu


Waziri wa Habari wa Somalia Mustafa Dhuhulow

VIKOSI vya serikali Somalia vimefanikiwa kuidhibiti upya Ikulu ya rais katika mji mkuu Mogadishu baada ya wapiganaji wa Al Shabaab kuishambulia.

Maafisa wanasema washambuliaji wapatao watano kutoka kundi la al-Shabab - waliuawa walipoingia katika eneo la ikulu hiyo.
Washambuliaji hao wanadaiwa kulipua bomu lililotegwa kwenye gari karibu na langu kuu la Ikulu hiyo.
Waziri wa habari na mawasiliano wa Somalia Mustaf Dhuhulow ameviambia vyombo vya habari kuwa tayari mmoja wa washambuliaji hao amekamatwa na anahojiwa na polisi.


No comments:

Post a Comment