![]() |
| Rais Barack Obama |
RAIS Obama anaomba dola bilioni 3.7 za msaada wa dharura kutoka
bunge la Marekani kusaidia kukabiliana na ongezeko la watoto waliohama peke yao
kutoka Amerika ya kati.
Ikulu ya Marekani inasema fedha hizo
zitasaidia kupunguza kile maafisa wanakitaja kuwa hali ya dharura ya
kibinaadamu iliyoshuhudia watoto zaidi ya elfu hamsini na mbili waliohama peke
yao kutoka El Salvador, Guatemala na Honduras kuvuka kiharamu mpaka wa Marekani
tangu mwezi Oktoba mwaka jana
Umaskini na ongezeko la hivi
karibuni la ghasia zinazohusiana na magenge na mitandao ya ulanguzi madawa ya
kulevya zimesababisha ongezeko la wahamiaji kutoka eneo hilo la Amerika ya
kati.
Wengi wao watoto ambao wameingia Marekani kupitia bonde la Rio Grande huko Texas.

No comments:
Post a Comment