Wednesday, July 9, 2014

WALEMAVU Kisarawe waomba kujengewa msikiti



 
Walemavu wakiwa nje ya msikiti jijini Dar
JUMUIYA ya Uchumi na maendeleo ya maendeleo ya walemavu JUMAWATA imeziomba Taasisi mbalimbali nchini kuwajengea msikiti na kuwachimbia kisima cha maji walemavu waishio kijiji cha Mtamba wilayani Kisarawe , mkoa wa Pwani  ili kuondokana na adha ya maji ya muda mrefu.

Akiongea na Mbiu ya Maendeleo wilayani Kisarawe mapema leo, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mshamu Mzanda amesema, jumawata iliamua kuomba ardhi kwajili ya shughuli za kilimo na ufugaji ili kujikomboa kiuchumi baada ya adha ya muda mrefu ya kuishi kama ombaomba jijini Dar es salaam toka mwaka  2004, lakini mpaka sasa hawana uhakika wa kupata maji kwani wanatembea umbali wa kilomita saba kufuata huduma hiyo.
Kuhusu msikiti amesema , jumuiya hiyo ni ya watanzania wenye itikadi za ukristo na uislamu, lakini kwa upande wa waislamu hawana sehemu ya kufanyia ibada  ilihali kwa upande wa wakristo wamepata mfadhili toka nchini  Korea ambaye amewajengea kanisa na shule.
Kutokana na hali hiyo amewahimiza wadau mbalimbali wa maendeleo kufika kijijini hapo ili waweze kuwasaidia waislamu kupata msikiti sanjari na ujenzi wa visima vya maji.   

No comments:

Post a Comment