Monday, August 11, 2014

WANANCHI waipongeza wizara ya afya kuzuia uuzwahji wa dawa katika nyumba za ibada


Waziri wa Afya na ustawi wa jami Dk Seif Rashidi

BAADHI ya  wananchi jijini Dar es salaam wameipongeza wizara ya Afya na ustawi wa jamii kwa hatua yake ya kuzuia uuzwaji wa dawa za binadamu katika nyumba za ibada.
Wakionhea na waandishi wa habari jijini Dar es salaama mapema leo, baadhi ya wanunuzi wa dawa zinazouzwa katika misikiti mbalimbali jijini Dar  wamesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya watu kujitambulisha kama madakatari bingwa wa baadhia ya magonjwa ilihali hawana hata elimu ya ngazi ya cheti juu ya mambo ya utabibu.
Hata hivyo wameitaka wizara husika kutoishia kwa wauzaji dawa wa misikiti bali  iende mbali zaidi hata kwa waganga wa jadi ambao nao wanafanyabiashara katika maeneo mbalimbali hapa nchini ,  baadhi yao  hawana taaluma ya utabibu wala udaktari.
                                                                











No comments:

Post a Comment