Tuesday, September 16, 2014

BUNGE la katiba lafungwa baada ya muda kumalizika


Waujmbe wabunge la katiba 

HABARI kutoka Dodoma Tanzania katika vikao vya Bunge maalumu la Katiba zinasema kuwa, majadiliano ya bunge hilo yamefungwa baada ya muda wa kufanya hivyo kumalizika.

Taarifa zaidi zinasema kuwa, keshokutwa Alkhamisi ndiyo siku ambayo rasimu ya mwisho inayopendekezwa na Bunge Maalumu la Katiba, itatolewa hadharani mbele ya Bunge hilo na Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi, Andrew Chenge.
Jana kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta, ndio ilikuwa siku ya mwisho ya majadiliano.
Leo Jumanne na kesho Jumatano, hakutakuwa na vikao vya Bunge, badala yake wajumbe wote watakutana kwenye semina mbalimbali, ikiwemo iliyoandaliwa na Bunge hilo wakati wanasubiri Katiba mpya kuwasilishwa bungeni.

No comments:

Post a Comment