Wednesday, September 10, 2014

KENYA yaahidi msaada wa shilingi bilioni 87 kusaidia mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ebola

Rais wa Kenya Uhuru Kenya 
KENYA  imesema kuwa itatoa msaada wa shilingi milioni 87 kwa Sierra Leone, Guinea na Liberia ili kusaidia mapambano dhidi ya ugonjwa wa ebola.
Hayo yalisemwa jana na Rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta. Rais wa Kenya amesema kuwa nchi yake imetoa mchango huo katika fremu ya sera za nje za Kenya za kushirikiana na nchi nyingine za Kiafrika.

 Rais Uhuru Kenyatta pia amewahakikishia Wakenya kuwa uchunguzi wa mipakani utaendelea ili kuhakikisha kuwa raia wa nchi hiyo wanalindwa na maambukizi ya ebola. Rais Kenyatta aliwahi kusema kuwa Kenya haitazitelekeza nchi za magharibi mwa Afrika zilizoathiriwa na homa hatari ya ebola. 

No comments:

Post a Comment