Tuesday, September 16, 2014

WANAJESHI kumi na wawili wapewa adhabu ya kifo kwa uasi






Wanajeshi nchini Nigeria
WANAJESHI  kumi na wawili nchini Nigeria wamepewa adhabu ya kifo kwa uasi pamoja na jaribio la mauaji.

Hii ni baada ya kumfyatuliwa bunduki afisa mkuu anayeongoza operesheni ya kupambana dhidi ya kundi haramu la kiislamu la Boko Haram kati mji wa Maiduguri,kaskazini Mashariki mwa nchi, mwezi wa Mei.
Wanajeshi wengine watano waliachiliwa baada ya ushahidi kukosekana.
Wanajeshi hao 12 walipatikana na hatia ya kumfyatulia risasi Jemedari amadu Mohammed.
Wanajeshi hao walikasirishwa na kamanda wao ambaye walimlaumu kwa kukataa kuchukua hatua baada ya msafara wao kushambuliwa.
Jeshi la Nigeria limeshindwa kuwashinda Boko Haram na wanajeshi wamekuwa wakilalamika kuwa kila wanapokabiliana na wapiganaji wa Boko Haram hawana silaha za kutosha kukabiliana nao.
Wote walikana mashtaka hayo katika Mahakama ya kijeshi mjini Abuja.
Kitengo hicho cha Jeshi ndicho kinakabiliana na Boko Haram
Mahakama ya kijeshi ya watu tisa ilisikiza kuwa tukio hilo lilitendeka baada ya kufyatuliwa kwa risasi kwa afisa mkuu wa kitengocha 7 cha jeshi la Nigeria.





No comments:

Post a Comment